WAKATI Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda akieleza kuwa ameagiza Serikali ya Mkoa wa Arusha kuzuia tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile, Kaimu Mkuu wa Mkoa huo, Raymond Mushi amesema ni vigumu kusitisha huduma hiyo.Mushi alisema pamoja na kutopata barua yoyote inayomwagiza asimamishe huduma za mchungaji huyo, ni vigumu katika mazingira yaliyopo katika Kijiji cha Samunge, Loliondo kufanya hivyo ikizingatiwa kwamba hivi sasa kuna maelfu ya watu hasa wagonjwa walioko hapo na wengine wakiendelea kumiminika. Soma zaidi HAPA |
No comments:
Post a Comment